
"Ili tuishi kwa amani ni lazima tutii sheria na kama hutaki kutii sheria tutashughulika naye, Kama kuna mtu anataka kuvunja amani katika mkoa wetu ajue kabisa hatoweza na niseme tu kwamba kama wanataka kujenga ukuta wajenge ukuta mwingine maana huu umeshadondoka".–Kamanda Sirro.
Aliongeza kwa kusema kuwa na wapo watu wanasema kwanini tunafanya mazoezi, nikwamba Jeshi la Polisi ni kawaida kufanya hivyo na muhimu watu wajue hiyo September 1 hakutakuwa na maandamano ya aina yoyote kwahiyo watu wasiwe na hofu bali wachape kazi.