1.0 UTANGULIZI
Kumekuwepo na taarifa zilizotolewa kwenye mitandao ya kijamii na vyombo vya habari, hasa gazeti la Jamboleo toleo namba 2541 la 23 Agosti, 2016 kuhusu Bodi ya Mikopo kuwadai wasionufaika na mikopo. Taarifa hizi zinalenga kuleta hofu na mkanganyiko usiokuwa wa lazima kwa wadau. Kufuatia hatua hiyo Bodi ya Mikopo inapenda kutoa ufafanuzi wa suala hili kama ifuatavyo:-