Quantcast
Channel: LEWIS MBONDE BLOG
Viewing all articles
Browse latest Browse all 7853

BREAKING NEWZZ:Koffi Olomide ahukumiwa kifungo cha miezi 18 jela

$
0
0
Mwanamuziki maarufu nchini Jamhuri ya Kidemokrasi ya Kongo, Koffie Olomide, amehukumiwa kifungo cha miezi 18 jela.
CoTRfBAWEAEvS2x

Koffi akiwasili kwenye gereza la Makala, Kinshasa kutumikia kifungo

Hukumu hiyo imekuja baada ya wiki iliyopita kusambaa kwa video inayomuonesha akimpiga teke dancer wake wakati wakiwasili kwenye uwanja wa ndege wa JKIA jijini Nairobi alikokuwa atumbuize Jumamosi iliyopita.
CoTRmOOXgAEtBGY

Tukio la kumpiga teke dancer wake limeteka vichwa vya habari duniani mwishoni mwa mwezi huu

Kufuatia tukio hilo alifukuzwa nchini humo na show yake kusitishwa. Show nyingine aliyokuwa aifanya nchini Zambia ilisitishwa siku chache baadaye.
CoTRihzWEAATy7p
Kwa mujibu wa mtandao wa Voice of Congo, hukumu hiyo imependekezwa na mwanasheria mkuu wa serikali. Staa huyo alikamatwa nyumbani kwake wiki hii.
CoTRp-WWIAARFHi
Japokuwa bado hakujatoka taarifa ya kina, imedaiwa kuwa hukumu hiyo haina faini ikimaanisha kuwa Olomide lazima aende jela
bongo 5

Viewing all articles
Browse latest Browse all 7853

Trending Articles