Quantcast
Channel: LEWIS MBONDE BLOG
Viewing all 7853 articles
Browse latest View live

Peter Okoye atangaza kurejea kwa P-Square, wamrudisha kaka yao kama meneja

$
0
0
Baada ya miezi kadhaa ya mfarakano wa ndani kwa ndani, kundi la P-Square limerejea.
12940912_1799083410377084_825748254_n
Member wa kundi hilo, Peter Okoye ametangaza kuwa wamemaliza tofauti zao na yote yaliyopita wameyaacha yapite. Peter amedai kuwa walijaribu kila mmoja kushika njia yake lakini wameshindwa.
Amewaomba radhi mashabiki wao na kusema anawajibika kwa yaliyotokea. Pia ametangaza kumrejesha kaka yao, Jude Okoye kama meneja wao.
Soma zaidi hapo chini alichoandika Peter kwenye Instagram:
My dear fans, P-Square is back. Ours is a journey that started from our mother’s womb. It was a journey that started from Primary School, continued to St. Murumba College, to when we were in University in Abuja. It was a journey in which we shared childhood memories and grown-up dreams. We are back because brothers do not let each other wander in the dark alone. We are back because we have tried the lonely road and it was not the same.
I want to take responsibility for what has happened and sincerely apologise to you our fans. For supporting us throughout this journey we owed you so much more than what you have had to endure and I apologise for that. We are embarking now on a new journey with exciting new management (Jude Okoye), new music and new ideas.
We cannot thank you enough for all your prayers and support throughout this difficult period. Maya Angelou once said that brotherhood is a condition that people have to work at. We will continue to work on that and you can be prepared to be blown away by this new phase of P-Square.
God bless you all and be assured that you have not seen anything yet!


MAHAKAMA KUU KANDA YA IRINGA YAMTIA HATIANI MTUHUMIWA WA MAUWAJI YA MWANAHABARI MWANGOSI

$
0
0
 Ulinzi  wa  polisi  viwanja  vya  mahakama  kuu kanda  ya  Iringa  leo  kabla ya  mtuhumiwa wa mauwaji  kufikishwa.
 Wananchi  wakiwa  foleni  kukaguliwa  kabla ya  kuingia  mahakamani leo.

 Mtuhumiwa wa  mauwaji  ya  Mwangosi  akipakiwa  kwenye  gari  za  FFU
 Msafala  wa  gari  za  FFU  zilizomsindikiza askari  mwenzao anayekutwa  na kosa  la  kuua bila  kukusudia  leo
 Askari  wa FFU  wakitoka  mbio  mahakamani  hapo
 Wananchi  na  wanahabari  wakitoka  mahakamani  hapo 

Wakili  kutoka mtandao  wa  watetezi wa haki  za  binadamu ((THRDC), Benedict  Ishabakaki  akizungumza na  wanahabari  nje ya  viwanja  vya mahakamani  leo
 Askari  hao  wakimtoa mahakamani  hapo  leo  mtuhumiwa wa mauwaji ya  Mwangosi

Na  MatukiodaimaBlog Iringa

 MAHAKAMA   kuu  kanda  ya  Iringa   imemtia hatiani   kwa   kosa la  kuua bila  kukusudia  askari  Polisi Kikosi cha Kutuliza Ghasia ( FFU )Iringa  G 58 Pacificius Cleophace Simon (27) anayetuhumiwa  kuuua  mwaahabari  Daudi  Mwangosi   mwaka 2012 katika  kijiji  cha  Nyololo  wilaya ya  Mufindi.

Hata   hivyo  mahakamani  hiyo  imesema  adhabu  kwa  mtuhumiwa   huyo  kutokana  na kupatikana na  kosa  hilo la  kuua bila  kukusudia  itatolewa  Julai 27  majira ya  saa 4  asubuhi  mwaka   huu.


 Jaji  Dkt  Paul Kiwelo ambaye  anayesikiliza  kesi  hiyo alisema  mahakakamani hapo jana   kuwa kati  ya  vielelezo  vitano vyote  vilivyoleta  kama  ushahidi  mahakamani  hapo  kwa ajili ya  kesi   hiyo  namba 54 ya  mwaka 2013  ni  kielelezo   kimoja  pekee  cha  ungamo  kwa  mlinzi  wa amani  ambacho  ndicho  hakukuwa na  shaka   na ungamo  hilo  ndilo  lililomtia hatiani  asikari  huyo.


Alivitaja   vielelezo vilivyopelekwa kama  ushahidi   kuwa ni Ramani   ya  eneo la  tukio,ripoti  ya  tabibu ,ungamo  la mlinzi  wa amani ,silaha  aliyoitumia  na  rejista  ya  silaha.

Noti na Sarafu za Shillingi 500 zatoweka

$
0
0
NOTI na sarafu ya Sh 500 zimeadimika kwenye mzunguko wa fedha kwa zaidi ya mwezi sasa, hali inayosababisha adha kubwa kwa wafanyabiashara,imefahamika.

Wakizungumza kwa nyakati tofauti   mwishoni mwa wiki, baadhi ya wafanyabiashara na makondakta wa mabasi ya daladala, Dar es Salaam, walieleza kuwa kukosekana kwa noti na sarafu ya Sh 500 kunasababisha usumbufu na kuongeza ugumu   katika kurudisha chenji kwa wateja.

Majidi Seifu ambaye ni kondakta wa daladala linalofanya kazi kati ya Kariakoo na Temeke, alisema mbali na kuadimika, noti za 500 zilizopo kwenye mzunguko zimechakaa kwa kiasi kikubwa.

“Noti na sarafu ya Sh 500 imekuwa ngumu kupatikana na kusababisha usumbufu mkubwa kwetu na abiria hususan wakati wa asubuhi.

“Hutulazimu kununua chenji kwa gharama kubwa na kutusababishia hasara  na uchelewaji vituoni,” alisema Seifu na kuongeza:

“Kama ukibahatika kupata noti hiyo inakuwa imechakaa sana na hata ukimpa abiria anaikataa huku  wauza chenji wakipandisha kiwango kutoka  Sh 4,500 hadi  Sh 4,700 kwa noti ya Sh 5000,” alisema Seif.

Mfanyabiashara wa kuuza chenji katika eneo la  Kariakoo, Orimpora Hussein, alisema  upatikanaji wa fedha hizo kwa kwa sasa ni mgumu tofauti na awali kwa vile  inaweza kupita siku siku nzima bila kushika noti wala sarafu ya Sh 500.

“Kawaida kuuza chenji ndogo kama 100 au 200 kwa  Sh 1,000 unauza kwa Sh 800 na chenji ya  50 au 100 ni Sh 700  ikiwa ni bei ya kawaida.

“Kutokana kuadimika kwa noti na sarafu hizo ni fursa kwetu maana chenji ya Sh 5,000 tunauza kwa Sh 4,500 na fedha hizo naona zinazidi kupotea katika mzunguko wa kila siku,” alisema Orimpora.

Alipoulizwa kuhusu hali hiyo, Mkurugenzi wa Huduma za Benki kutoka Benki Kuu ya Tanzania (BoT), Marcian Kibello, alisema noti za Sh 500 hazitakuwapo katika mzunguko wa fedha kwa vile hazitatengenezwa tena.

“Tangu tulipoitambulisha sarafu ya Sh 500 Oktoba 2014 hatujatengeneza noti tena kwa sababu  zinachakaa na kuharibika mapema ingawa wananchi wanazikataa sarafu.

“Ila sarafu zinapunguza gharama kwa vile zinadumu tofauti na   noti.

“Nashauri taasisi za fedha kuhakikisha zinasambaza sarafu hizo katika mzunguko wa fedha na pia wananchi wazizoee kwa matumizi na  wazichukue sarafu hizo katika benki mbalimbali  kuhakikisha zinakuwapo katika mzunguko,”alisema Mkurugenzi huyo.

Kibello aliwakumbusha wananchi kuwa BoT inatoa huduma ya chenji za sarafu ya Sh 500 kila siku za Jumanne na Alhamisi hivyo wananchi na wafanyabiashara watumie fursa hiyo kuzipata.

Magazeti ya Leo Tanzania Jumanne ya July 26,2016

Mshtakiwa wa Kuiba Milioni 7 kwa dakika Aongezewa Kesi Nyingine

$
0
0

TAASISI ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru) leo inatarajiwa kuwapandisha kizimbani wafanyabiashara wawili akiwemo Mohamed Mustafa Yusufali ‘Choma’ aliyewahi kutajwa kuwa anajipatia Sh milioni saba kwa dakika moja kwa njia za udanganyifu katika mapato ya serikali.

Choma na mfanyabiashara wa Arusha, Samweli Lema, walifikishwa katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, Dar es Salaam jana saa 9 mchana kwa ajili ya kusomewa mashitaka yanayowakabili, lakini ilishindikana kwa sababu muda ulikuwa umekwisha.

Washtakiwa hao waliondolewa katika viwanja vya mahakama hiyo jioni na kurudishwa mahabusu kwa kutumia magari ya Takukuru, hivyo leo wanatarajiwa kupandishwa kizimbani kwa ajili ya kusomewa mashitaka yao.

Choma atakuwa anakabiliwa na kesi mbili kwa wakati mmoja, kwa kuwa Julai 12 mwaka huu, alifikishwa mahakamani hapo na wenzake wakikabiliwa na mashitaka 199 likiwemo la kuisababisha serikali hasara ya Sh bilioni 15.6.

Awali kesi ya kuisababishia serikali hasara ya Sh bilioni 15.6 inayomkabili Choma na wenzake Alloyscius Gonzaga Mandago, Isaack Kasanga, Taherali Sujjauddin Taherali na Mohamed Kabula ilitajwa mbele ya Hakimu Mkazi Mkuu Huruma Shahidi.

Wakili wa Serikali Mwandamizi, Mutalemwa Kishenyi alidai kuwa upelelezi wa kesi hiyo haujakamilika, hivyo anaomba tarehe nyingine kwa ajili ya kutajwa. 

Aidha, aliiomba Mahakama iwaruhusu kumchukua Choma kwa ajili ya kumhoji kutokana na tuhuma mpya zinazomkabili na kuahidi kumrudisha mahakamani kabla saa za kazi hazijaisha.

Baada ya kueleza hayo, Hakimu Shahidi alimuuliza mshtakiwa huyo kama ana lolote la kusema, alikaa kimya lakini baadaye alidai kuwa ameelewa na atakuwa tayari endapo wakili wake atakuwepo kwenye mahojiano hayo.

Hakimu Shahidi aliruhusu upande wa Jamhuri umchukue mshtakiwa huyo na kuahirisha kesi hiyo hadi Agosti 5, mwaka huu. 

Choma ambaye pia ni Mkurugenzi wa Kampuni ya Superior Financing Solution Limited kwa mara ya kwanza alifikishwa mahakamani hapo Julai 12, mwaka huu akikabiliwa na mashitaka 199 ya kughushi, kuwasilisha nyaraka za uongo, uhujumu uchumi utakatishaji fedha na kuisababishia serikali hasara ya Sh bilioni 15.6.

Katika mashitaka ya kughushi inadaiwa alighushi hati za usajili kuendesha kampuni 15 ikiwemo Festive General Business Limited zimesajiliwa kihalali nchini jambo ambalo si kweli. Aidha, anadaiwa kuwasilisha nyaraka hizo za kughushi kwa Kamishna wa Kodi Ofisi za TRA Mkoa wa Kinondoni ili kuonesha kampuni hizo zimesajiliwa na zinastahili kusajiliwa kama mlipa kodi.

Mbali na mashitaka hayo, washtakiwa wote wanadaiwa kutakatisha fedha, kwa kuficha uhalali, chanzo na mzunguko wa Sh 1,895,885,000 kwa kuzikopesha fedha hizo kwa watu mbalimbali na kupokea marejesho ya mikopo huku wakijua fedha hizo zimetokana na njia zisizo halali za kughushi na kukwepa kodi.


Yusufali anadaiwa kati ya Januari 2008 na Januari mwaka huu, kwa vitendo viovu vya kughushi na kuwasilisha nyaraka za uongo kwa Kamishna wa TRA, ameisababishia serikali hasara ya Sh bilioni 15.6 ambazo zilitakiwa kulipwa kama Kodi ya Ongezeko la Thamani (VAT).

Mchungaji Anthony Lusekelo Adai Lowassa ni Tishio CCM......Asema Uchaguzi Umekwisha, si Busara Kuendelea Kumpiga Vijembe

$
0
0


Mchungaji wa Kanisa la Maombezi (GRC) la Ubungo jijini Dar es Salaam, Anthony Lusekelo maarufu ‘Mzee wa Upako’ amesema kitendo cha viongozi wa CCM kulitaja zaidi jina la Edward Lowassa katika Mkutano Mkuu Maalumu wa chama hicho ni ishara kuwa Waziri Mkuu huyo wa zamani ni tishio.

“Nani! Lowassa…. jina lake kutajwa sana katika vikao vya CCM. Hiyo inaashiria kuwa ni mtu tishio. Ndiyo ni tishio,” alisema Lusekelo jana katika mkutano wake na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam.

Lusekelo ambaye hivi karibuni, Rais John Magufuli alishiriki ibada katika kanisa lake, alimzungumzia Lowassa baada ya kuulizwa swali juu ya mtazamo wake kuhusu Mkutano Maalumu wa CCM ambao jina la mgombea huyo wa urais kupitia Chadema na Ukawa lilitajwa na makada wengi wa chama hicho tawala.

Alisema hilo lilidhihirika hata katika mchakato wa CCM kupata mgombea wake wa urais, kutokana na Lowassa kuungwa mkono kwa kiasi kikubwa.

Alisema kitendo cha Waziri Mkuu huyo wa zamani kuzua mjadala katika Mkutano Mkuu wa chama hicho tawala sambamba na wimbi la makada wanaohama vyama vyao, si mambo yanayopaswa kuwa mjadala kwa sababu uchaguzi ulishapita.

Huku akisema: “Sizungumzi haya kwa ajili ya kujipendekeza, sihitaji ukuu wa wilaya,” Lusekelo aliwataka viongozi kukataa kuendeleza uhasama wa kisiasa na chuki kwa maelezo kuwa mwaka huu uwe maalumu kuzika tofauti hizo, kufanya kazi kulijenga Taifa na kuhubiri amani na umoja.

Katika mkutano huo, Lusekelo alipongeza kuimarika kwa vyama vya upinzani akaponda mvutano ulioibuka bungeni akisema kukosa uzoefu kwa Naibu Spika, Dk Tulia Ackson kulichangia huku akiunga mkono kauli ya Rais kuzuia shughuli za siasa na kubainisha jinsi Rasimu ya Katiba ya Tume ya Jaji Joseph Warioba, ilivyopendekeza kupunguzwa kwa madaraka ya Rais.

Jumamosi iliyopita, katika Mkutano Mkuu wa CCM mjini Dodoma, uliomalizika kwa Rais Magufuli kuchaguliwa kuwa mwenyekiti, mzimu wa Lowassa ulitawala kutokana na kila aliyepewa nafasi ya kuzungumza ama kumtaja kwa jina au kwa mafumbo.

Mwenyekiti wa CCM aliyemaliza muda wake, Jakaya Kikwete ndiye aliyeanza kuzungumzia hali ya mchakato wa chama hicho kupata mgombea wake wa urais, kuwa ulikuwa mgumu na majaribu makubwa na kwamba wazee walifanya kazi kunusuru hali hiyo.

Katika mchakato huo, CCM ilikata jina la Lowassa katika hatua za awali, jambo lililosababisha kiongozi huyo kuhama na kundi la wanaCCM na kujiunga na Chadema ambayo ilimteua kuwa mgombea wake wa urais.

Hata hivyo, katika mkutano wake wa jana, Lusekelo alisema katika mchakato wa chama hicho tawala kupata mgombea wake wa urais kulikuwa na watu wenye majina makubwa, akiwamo Lowassa na aliyekuwa Waziri wa Mambo ya Nje, Bernard Membe.

“Niliwaambia CCM, Membe huwezi kumpuuza, Lowassa naye huwezi kumpuuza maana wanataka madaraka na kwa vyovyote lazima mtapata mtikisiko. Nikawaomba waahirishe suala la kupata Katiba Mpya maana wasingelimaliza na muda ulikuwa mfupi,” alisema na kuongeza: “Kama mwaka huu hautatumika kutibu majeraha yaliyotokea huko nyuma, tutaharibikiwa sana.”

Alisema mchakato wowote wa uchaguzi na kura ya maoni ndani ya vyama huacha mpasuko na watu hutumia dini na ukabila kubaguana, hivyo lazima baada ya uchaguzi mambo hayo yamalizwe.

“Tunapaswa kukumbuka kuwa wote ni Watanzania tusahau uchaguzi. Sasa ni wakati wa kuijenga nchi. Amani inatengenezwa, na Mungu huwapa hekima maana kujenga ni kazi na kubomoa ni rahisi, huu ni mwaka wa uponyaji na kurejesha Taifa pamoja,” alisema Lusekelo.

Alisema kuanza kubagua watu kwa sababu walitoka CCM kwenda Chadema au kutoka Chadema kwenda chama tawala si jambo sahihi huku akitolea mfano mataifa yaliyovurugika kwa kuendekeza siasa za chuki na uhasama.

Yaliyotokea bungeni
Akizungumza yaliyotokea bungeni na kusababisha wabunge wa Ukawa kususia vikao vya Bunge vilivyoongozwa na Dk Tulia, Lusekelo alisema Mtanzania anayejua historia ya nchi yake hawezi kufumbia macho suala hilo.

“Binafsi nawalaumu waliotoka (wabunge wa upinzani) na waliobaki (wabunge wa CCM). Kushindana si kuzuri. Mbatia (James Mbunge wa Vunjo na Mwenyekiti wa NCCR-Mageuzi) na wenzake wanapaswa kujua kuwa naibu spika ni mchanga katika siasa waende naye taratibu maana kapewa ubunge tu na kuwa naibu spika,” alisema.

Huku akiponda uamuzi wa Serikali kufuta urushwaji wa matangazo ya moja kwa moja ya Bunge alisema: “Nashangaa wazee kama Salim (Ahmed Salim – Waziri Mkuu mstaafu), Pinda (Mizengo – Waziri Mkuu mstaafu) na Warioba. Sijui walishindwa nini kukaa na wabunge hawa ili kumaliza tofauti zao.”

Alisema si jambo jema kuongoza nchi kwa mabavu na kusisitiza kuwa hata uhuru ulipatikana kwa mazungumzo.

Mchungaji huyo aliusifu utawala wa Rais Magufuli kuwa una kasi kubwa na kwamba licha ya wananchi kulia ukata, watacheka baada ya mwaka mmoja huku akiwananga wanaomponda Kikwete kuwa hawajui mazuri aliyoyafanya.

Awapongeza wapinzani
Akizungumzia nguvu ya vyama vya upinzani, Lusekelo alisema ushindani wa kisiasa umekuwa mkubwa kutokana na kuimarika kwa upinzani: “Chadema ya sasa si ile ya miaka ya 1990. Wanaongoza miji mikubwa na ukiona chama kina wabunge 40 usikipuuze. Hata nguvu ya mfalme ni watu.”

Mikutano ya siasa
Kuhusu kauli ya Rais kusitisha shughuli za siasa hadi mwaka 2020, alisema jambo hilo linaweza kuonekana baya lakini lina unafuu mkubwa, kwamba Kenya wamelifanya na kufanikiwa kumaliza tofauti za kisiasa.

“Hivi watu 10,000 wakiandamana na kusema Magufuli aliiba kura itakuwaje? Tuna askari wa kuwazuia! Nadhani wanasiasa wafanye kazi ya utawala katika vyama vyao. Tutulie kwanza tutibu majeraha. Hakuna jambo baya kama kuwaongoza watu wenye njaa maana hawana la kupoteza,” alisema.

Hata hivyo, Lusekelo alisema Rasimu ya Katiba ilipendekeza Rais kupunguziwa madaraka na huenda madaraka makubwa aliyonayo Rais yakawa sababu ya nchi kuendelea kuwa na amani.

“Kenya kuzuia maandamano ni ngumu sana lakini hapa kwetu hadi Zitto (Kabwe-Kiongozi wa ACT-Wazalendo) alizuiwa kufanya mkutano wa ndani. Kwetu rais ana madaraka makubwa sana,” alisema huku akiwataka polisi kutekeleza wajibu wao vyema, wakikumbuka kuwa nao ni binadamu.

Makongoro Nyerere Anusurika Ajalini....

$
0
0
Mbunge wa Bunge la Afrika Mashariki, Makongoro Nyerere amenusurika katika ajali baada ya gari lake kuwagonga ng’ombe saba kwenye eneo la Makatanini, Babati mkoani Manyara.

Mtoto huyo wa Baba wa Taifa, Mwalimu Julius Nyerere, alikuwa anatoka Dodoma kwenye mkutano mkuu maalumu wa CCM uliomchagua Rais John Magufuli kuwa mwenyekiti wa tano wa chama hicho kwenda Arusha.

Kamanda wa polisi wa mkoa wa Manyara, Francis Massawe amesema ajali hiyo ilitokea saa 1 usiku jana na kuwaua ng’ombe saba na kondoo mmoja.

Amesema chanzo cha ajali hiyo ambayo haikuwa na madhara ya binadamu, ni mifugo hiyo kuvushwa barabara sehemu isiyo na kivuko rasmi cha mifugo na katika tukio hilo. Mchungaji wa mifugo hiyo, William German alikimbia baada ya ajali hiyo. 

JULY 28 BIRTHDAY JOINT AT MAISHA BASEMENT COME SHARE CAKE WITH DR CHENI


Kikwete: Nashukuru Mungu Kwa Kuutua Mzigo Salama Huku Nikiiacha Nchi Ikiwa Salama Tulii Kabisa

$
0
0

MWENYEKITI Mstaafu wa Chama cha Mapinduzi CCM Dkt.Jakaya Kikwete amesema anashukuru Mungu Kwa kuutua mzigo salama huku akiicha nchi ikiwa salama tulii kabisa.

Amesema kuwa safari yake ya urais ilianzia Bagamoyo akitokea wilayani hapo ambapo baada ya hapo alikwenda Kibaha kutangaza nia ya kugombea urasi nakudai kuwa amejisikia furaha kurudi tena Bagamoyo akiwa salama.

Amesema wakati akielekea kutangaza nia ya kugombea urais alikuwa na mtoto wake Ridhiwani Kikwete ambapo yeye alikuwa anaandika na Ridhiwani anachapa kwenye Komputa.

Dkt.Kikwete aliyasema hayo jana wilayani Bagamoyo katika hafla ya kumkaribisha Nyumbani baada ya kuitumikia nchi Kwa miaka mingi, ambapo iliandaliwa na Chama Cha Mapinduzi Mkoa wa Pwani.

Alisema anashukuru Kwa Mara nyingine kurudi mahala alipoanzia na kwamba amemaliza salama na ameacha nchi ikiwa salama na imetulia tulii kama Maji kwenye mtungi.

Akikumbuka mchakato wa mwaka jana wa kumpata Mgombea ulikuwa na mambo mengi lakini mambo yalikwenda salama na hakuna lililokuwa limeharibika .

"Ilikuwa Kazi kubwa si ndogo lakini hatimaye wa kavuka na wakaingia kwenye uchaguzi ambao ulikuwa na vurumai" alisema Dkt.Kikwete .

Aidha alisema kuwa hata hivyo katika uchaguzi huo kulikuwa hakuna mtu ambaye alipatwa na tukio la kumpiga mwezake hali ambayo iliwashangaza hata nchi jirani.

Alisema kuwa katika kipindi chake cha uongozi amefanya kazi kubwa ya kusukuma maendeleo ya wananchi Kwa mikoa yote,wilaya zote bila ubaguzi wowote ule huku akikiri kukabiliana na Changamoto ya kunyoshewa vidole hususani pale alipojaribu kupeleka maendeleo Wilayani Bagamoyo kanakamba wananchi wa Bagamoyo walikuwa hawana haki.

Aidha Dkt.Kikwete alisema kuna wakati alisimamisha fedha za ujenzi wa barabara hiyo na kupeleka fedha hizo kujenga barabara ya Geita, Sengerema,usagala ,na kulizuka na Maneno mengi dhidi yake na hadi kufikia wabunge kulumbana.

Alisema hata hivyo anashukuru kwamba amemaliza salama na Kwa bahati nzuri amepatikana rais ambaye ana ari kubwa ya kuwaletea maendelea watu huku akitaka watanzania kumuunga mkono.

BREAKING NEWZZ:Koffi Olomide ahukumiwa kifungo cha miezi 18 jela

$
0
0
Mwanamuziki maarufu nchini Jamhuri ya Kidemokrasi ya Kongo, Koffie Olomide, amehukumiwa kifungo cha miezi 18 jela.
CoTRfBAWEAEvS2x

Koffi akiwasili kwenye gereza la Makala, Kinshasa kutumikia kifungo

Hukumu hiyo imekuja baada ya wiki iliyopita kusambaa kwa video inayomuonesha akimpiga teke dancer wake wakati wakiwasili kwenye uwanja wa ndege wa JKIA jijini Nairobi alikokuwa atumbuize Jumamosi iliyopita.
CoTRmOOXgAEtBGY

Tukio la kumpiga teke dancer wake limeteka vichwa vya habari duniani mwishoni mwa mwezi huu

Kufuatia tukio hilo alifukuzwa nchini humo na show yake kusitishwa. Show nyingine aliyokuwa aifanya nchini Zambia ilisitishwa siku chache baadaye.
CoTRihzWEAATy7p
Kwa mujibu wa mtandao wa Voice of Congo, hukumu hiyo imependekezwa na mwanasheria mkuu wa serikali. Staa huyo alikamatwa nyumbani kwake wiki hii.
CoTRp-WWIAARFHi
Japokuwa bado hakujatoka taarifa ya kina, imedaiwa kuwa hukumu hiyo haina faini ikimaanisha kuwa Olomide lazima aende jela
bongo 5

Aliyebikiri wasichana 104 Malawi agundulika na ngoma na kukamatwa

$
0
0
Eric Aniva aliyeripotiwa wiki iliyopita huwa huingiza fedha kwa kazi ya kuwabikiri wasichana nchini Malawi amekamatwa na polisi nchini humo.
160721100547_aniva_the_hyena_624x351_bbc_nocredit
Aniva ambaye ni maarufu kwa jina la Fisi, hulipwa kiasi cha dola 7 na wazazi wa kabila moja huko nchini Malawi kwa ajili ya kuwabikiri watoto wao wa kike wakiamini kuwa mtoto wa kike kuwa na bikira na mkosi.
Baada ya taarifa hiyo kuruka kupitia BBC, Rais wa Malawi, Peter Mutharika kupitia kwa Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Ikulu ya nchi hiyo, Bright Molande aliamuru raia huyo akamatwe kutokana na vitendo hivyo vya uzalilishaji kwa watoto wa kike.
“And since Mr. Eric Aniva confesses to be HIV positive and that he never uses protection in his evil acts against the innocent girls and women, he should further be investigated for exposing the young girls to contracting HIV and further be charged accordingly,” alisema rais Mutharika.
“These practices not only cast a shadow on the hard-earned achievements my Government has made on issues such as violence and HIV prevention but they also go against a vision of development that seeks to ensure that the youth (and in particular young girls), are able to achieve their full potential.”
“Furthermore, these horrific practices although done by a few also tarnish the image of the whole nation of Malawi internationally and bring shame to us all,” aliongeza.
“ Children, girls and women must be cared for, protected and provided every opportunity to survive peacefully and become productive citizens.”
Aniva anakadiriwa kuwabikiri zaidi ya watoto wa kike 104 lakini kubwa zaidi amegundulika kuwa na virusi vya ugonjwa ukimwi na haijulikani ni watoto wangapi tayari amewaambukiza virusi hivyo.

CALL +255 658 194 194 FOR BOOKING MC KENYATTA

$
0
0

BOOK NOW MC KENYATTA

 CALL +255 658 194 194


BOOK NOW MC KENYATTA

 CALL +255 658 194 194



BOOK NOW MC KENYATTA

 CALL +255 658 194 194



BOOK NOW MC KENYATTA

 CALL +255 658 194 194

CALL +255 754 222 201 OR +255 658 194 194 FOR BOOKING MC DR CHENI

$
0
0

Mc Dr Cheni on the stage

For Booking Please Call

 Mc Dr Cheni

VODACOM: +255 754 222 201


Manager: Lewis Mbonde

Tigo: +255 658 194 194
a
 Lewis Mbonde

PIGA +255 717 344 281 AU +255 784 732 242 KUPATA HUDUMA YA DR MNINDO NI MTAALAMU BINGWA WA TIBA ASILI NA MBADALA

$
0
0

LEWIS MBONDE BLOG INADHAMINIWA NA DR MNINDO NI MTAALAMU BINGWA WA TIBA ASILI NA MBADALA.ANAPATIKANA MOROGORO,MTAA WA MAFISA KARIBU NA KANISA LA KAKOBE

PIGA 

+255 717 344 281
+255 765 732 242
+255 784 732 242

HUDUMA ANAZOZITOA

1.KUTOA MAJINI MWILINI


2.KUSAFISHA NYOTA NA KUPANDISHA


3.KUPATA KAZI KWA HARAKA NA KUPANDISHWA CHEO


4.KESI SUGU ZISIZOISHA


5.KUTIBU KIZAZI(KUPATA MTOTO)


6.KUTOA VIFUNGO MWILINI NA KINGA YA MWILI


7.KUTIBU KICHAA


8.KUMRUDISHA ALIYEPOTEA


9.NGUVU ZA KIUME KUKOSEKANA


10.VIDONDA VYA TUMBO


11.KUTIBU SUKARI


12.KUKOSA HAMU YA TENDO LA NDOA KWA MUME AU MKE

CALL +255 658 194 194 KUTANGAZA BIASHARA YAKO HAPA BEI ZETU NI NAFUU SANA

$
0
0


LEWIS MBONDE BLOG Audience: 

Readers of our blog 1,609,556

TANGAZO KUBWA LA JUU TOP AD BANNER 100,000/= KWA MWEZI

TANGAZO SIZE YA KATI  LA PEMBENI SIDER BANNER  80,000/= KWA MWEZI

TANGAZO DOGO 50,000/= KWA MWEZI


Demographics
The targeted audience is aged between 18 and Above
Lewis Mbonde blog is read in 130+ countries, but the targeted audience are the residence mainly in Tanzania.We have a good number of Audience from Unated State of America(USA),Europe,Africa e.g Kenya,Uganda,Burundi,Rwanda,Zambia,Malawi,South Africa,Bostwana,Zimbabwe,Ghana,Togo,Nigeria,Congo,Ethiopia etc
,Asia and Worldwide.
Lewis Mbonde Blog  Advertising Rates


Discount %

3 Month5 Month8 Month12 Month
Home PageSize@month10%11%12%14%
Home Page
Top Ad Banners960x250 px
100,000
270,0004450,000704,0001,032,000
Side Banners300×250 px
80,000
162,000267,000422,400   619,200







Post Title Banner640x90 px50,000135,000222,500352,000516,000

Advertising Options:
Standard Advertising
Text Ads and Video Ads (Price on enquiry)

Branded Advertising
Skins, watermarks, custom modules and navigation bars (Price on enquiry)

Sponsored Content
Dedicated section, sponsored articles, polls and competitions (Starts at 50,000 TShs. per month)

Social Media Sponsorship
On Facebook, Twitter and YouTube (Starts at 100,000 TShs. per month)Loading...  


Welcome advertise with us today

Kwa Maelezo zaidi usisite kutupigia/For more info please call

                              
                      +255 658 194 194

CALL +255 658 194 194 FOR LEWIS MBONDE IT & BUSINESS CONSULTANCY BLOG DESIGNING,GOOGLE ADSENSE,BLOG MODIFICATION, LOGO DESIGNING,RESEARCH PROPOSAL WRITTING,RESEARCH PAPER WRITING,PROJECT PROPOSAL ETC

$
0
0
  

                         CALL +255 658 194 194
  
                 BLOG DESIGNING (BLOG YA KISASA)
             BLOG MODIFICATION (KUIBORESHA BLOG)
                 ADSENSE (BLOGGER UJIPATIE KIPATO)
              LOGO DESIGNING
              WEBSITE DESIGNING
              DOMAIN NAME REGISTRATION
              PROJECT PROPOSAL 
              KUANDAA KATIBA ZA NGO NA KIKUNDI
              COMPANY PROFILE
              RESEARCH PROPOSAL WRITTING
                   RESEARCH PAPER WRITING
              BUSINESS IDEA (KUTOA WAZO LA BIASHARA)
              FINANCIAL STATEMETS EXCEL TEMPLATE 
              FINANCIAL STATEMENTS PREPARATION 
              ACCOUNTING SOFTWARES
              WEBSITE HOSTING
              ENTREPRENEURSHIP ADVICE
              WEBSITE WITH DATABASE NEGOTIABLE

            

                            CALL +255 658 194 194

Magazeti Ya Leo Jumatano ya July 27,2016

BASI LA UDA LAGONGA TRENI ENEO LA GEREZANI – KARIAKOO JIJINI DAR

$
0
0

Ajali imetokea usiku wa leo kati ya treni na basi la Uda linalofanya safari zake kati ya Kariakoo na Mbagala na kuua mtu mmoja na wengine zaidi ya 45 kujeruhiwa.
Kaimu Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Kipolisi wa Ilala, Ernest Matiku amesema majeruhi wamepelekwa Hospitali ya Taifa ya Muhimbili kwa matibabu.
Hata hivyo, hakuweza kumtaja jina mtu huyo aliyefariki dunia.
“Ni kweli ajali imetokea kuna kifo cha mtu mmoja na watu wengi wameumia sana na hivi ninavyozungumza na wewe naelekea Muhimbili,” amesema Kaimu kamanda huyo.
 
Michuzi Blog

Mawakili zaidi ya 100 Waandamana kudai haki

$
0
0
MAWAKILI wa kujitegema zaidi ya 100 mkoani Arusha, jana waliandamana kwenda kwa Kamanda wa Polisi Mkoa wa Arusha, Charles Mkumbo, kulaani kile walichokiita ukandamizwaji wa sheria za nchi na kazi ya uwakili unaofanywa na polisi.

Wanasheria hao wanalaani kitendo cha wakili mwenzao, Shilinde Ngalula, kukamatwa, kufungwa pingu na kufunguliwa mashtaka akiwa kazini Loliondo wilayani Ngorogoro.

Mawakili hao walitembea zaidi ya hatua 400 kabla ya kuzingirwa na polisi ambao waliwataka kuunda kamati ya watu wachache kwenda kuzungumza na Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Arusha, Charles Mkumbo.

Uamuzi wa kufanya maandamano hayo, ulipitishwa jana mjini hapa baada ya mawakili hao kufanya kikao cha pamoja viwanja vya Mahakama ya Hakimu Mkazi Arusha.

Awali, mawakili hao wakiongozwa na Mwenyekiti wa Chama cha Mawakili Tanganyika (TLS), Wakili Modest Akida, pia walikubaliana kutoendelea na kesi za wateja wao waliokuwa mahakamani.

Akizungumzia maandamano hayo, Akida alisema yalilenga kupinga kitendo cha Jeshi la Polisi wilayani Ngorongoro, kumkamata na kumfungulia mashitaka Wakili Ngalula.

Wakiwa tayari wameandamana umbali wa takribani hatua 400 kutoka mahakamani hapo, vikosi vya askari polisi waliovalia kiraia na wale wa Kikosi cha Kutuliza Ghasia (FFU) wakiwa ndani ya magari mawili, waliwazunguka na kuwaamuru kusimama.

Mkuu wa Kituo Kikuu cha Polisi Arusha, Thomas Mareko, aliwataka wanasheria hao kufuata sheria katika kudai na kuwasilisha malalamiko yao.

“Nyinyi ni wanasheria, mpaka hapa tayari mmeshaandamana kinyume cha sheria za nchi, nawaomba chagueni wawakilishi nitawasindikiza mnakokwenda na wengine rudini mkaendelee na majukumu yenu,” alisema Mareko.

Baada ya maandamano hayo kuzuiwa, mawakili hao waliwachagua wawakilishi waliokwenda kuwasilisha malalamiko yao kwa Kamanda Mkumbo na wengine walirudi katika viwanja vya mahakama kusubiri taarifa.

Awali, akizungumza katika viwanja hivyo, Wakili George Njooka alisema mawakili nchini wameanza kudharauliwa na vyombo vya dola.

“Hawa watu walianza na vyombo vya habari, wakaenda kwa wanasiasa na sasa wamekuja kwa mawakili, nawaomba tuanzie hapa twende kwa RPC atuambie haya maelekezo tunayoambiwa yanatoka juu, yanatoka kwa nani,” alisema Wakili Njooka.


Wakili Qamara Peter aliwakumbusha mawakili wenzake kuwa haki siku zote haiombwi bali inadaiwa.

Aliyekuwa Akiibia Serikali Milioni 7 Kwa Dakika Asomewa Mashitaka Mapya 222

$
0
0
WAFANYABIASHARA wawili, akiwemo Mohamed Yusufali “Choma”, wamepandishwa kizimbani katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, wakikabiliwa na mashitaka 222 ya kuisababishia serikali hasara ya zaidi ya Sh bilioni 14.

Mbali na Yusufali aliyewahi kutajwa kuwa anajipatia Sh milioni saba kwa dakika moja kwa njia ya udanganyifu katika mapato ya serikali, mshitakiwa mwingine ni Mkurugenzi wa Kampuni ya Northern Engineering Works Limited, Samwel Lema, ambao wanadaiwa kusababisha hasara kwa kughushi na kukwepa kulipa kodi.

Washitakiwa walifikishwa mahakamani hapo jana na kusomewa mashitaka kwa zaidi ya saa tatu na Wakili Mwandamizi wa Serikali, Mutalemwa Kishenyi, akisaidiwa na Jackline Nyantori, Diana Lukondo na Wakili kutoka Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru), Leonard Swai.

Mbele ya Hakimu Mkazi Wilbard Mashauri, ilidaiwa, katika tarehe tofauti kati ya Januari Mosi 2012 na Desemba 31, 2014, washitakiwa hao na wengine ambao hawajafikishwa mahakamani walipanga njama za kuidanganya Mamlaka ya Mapato (TRA) na kujipatia Sh 14,052,011,435.

Wakili Kishenyi akisaidiwa na Nyantori walidai, katika shitaka la tano hadi 103 kuwa, kati ya mwaka 2011 na 2013, jijini Dar es Salaam na Arusha, washitakiwa hao walighushi stakabadhi za malipo kuonesha Kampuni ya Northern Engineering Works Ltd imenunua bidhaa mbalimbali.

Ilidaiwa kuwa stakabadhi hizo zilionesha kuwa kampuni hiyo imenunua bidhaa mbalimbali kutoka kwenye kampuni tofauti tofauti ikiwemo ya Festive General Business Ltd, Ever Global General Trading na Jambo Product Ltd, jambo ambalo si kweli.

Wakili Diana na Swai waliendelea kudai, katika shitaka la 104 hadi 141, kuwa kati ya mwaka 2011 na 2015, Lema alighushi hati ya Kodi ya Ongezeko la Thamani (VAT) kuonesha kuwa kampuni yake imenunua bidhaa mbalimbali kutoka kampuni tofauti tofauti ikiwemo ununuzi wa vifaa vya Sh bilioni 1.7.

Wakili Swai alidai katika shitaka la 142 hadi 219 kuwa, kwa lengo la kufanya udanganyifu washitakiwa hao walighushi stakabadhi za malipo kuonesha Kampuni ya Elerai Constructions Ltd, imenunua vifaa mbalimbali kutoka katika kampuni tofauti tofauti ikiwemo Kampuni ya Blue Arrow Tanzania Ltd.

Aliendelea kudai shitaka la 220, linamkabili Lema ambaye anadaiwa kati ya Januari Mosi, 2012 na Desemba 31, 2015, Dar es Salaam, akiwa Mkurugenzi anayehusika kushughulikia Kampuni yake ya Northern Engineering Works Ltd na Elerai Constructions Ltd zilizosajiliwa kama walipa kodi, aliwasilisha nyaraka za uongo.

Inadaiwa aliwasilisha nyaraka ambazo ni marejesho ya uongo ya Kodi ya VAT kwa Kamishna Mkuu wa TRA jambo lililosababisha akwepe kulipa kodi ya Sh bilioni 14,052,011,435. 
Katika mashitaka ya utakatishaji wa fedha, ilidaiwa kati ya Februari Mosi, 2012 na Februari 25, 2013 jijini Dar es Salaam na Arusha, washitakiwa hao walijihusisha na kuhamisha Sh milioni 420 zilizotokana na vitendo vya uhalifu.

Inadaiwa waliziingiza fedha hizo kwenye akaunti namba 1010000541 inayomilikiwa na Iqbal Jaferali Jafferjee iliyopo katika Benki ya I&M tawi la Kariakoo, na kuzitoa huku wakijua zimepatikana kwa njia za uhalifu ambazo ni kughushi na kukwepa kulipa kodi.

Iliendelea kudaiwa katika shitaka la 222 kuwa, kati ya Januari Mosi, 2012 na Desemba 31, 2015, Dar es salaam, kutokana na vitendo vyao vya kuwasilisha marejesho ya VAT ya uongo kwa Kamishna Mkuu wa TRA waliisababishia mamlaka hiyo hasara ya zaidi ya Sh bilioni 14.

Hakimu Mashauri aliwaeleza washitakiwa hao kuwa, hawaruhusiwi kujibu mashitaka yao kwa kuwa Mahakama hiyo haina mamlaka ya kusikiliza kesi za uhujumu uchumi isipokuwa Mahakama Kuu.

Baada ya kusomewa mashitaka, upande wa Jamhuri ulidai upelelezi wa kesi hiyo bado unaendelea na kuomba tarehe nyingine ya kutajwa, hata hivyo Wakili Alex Mgongolwa anayeongoza jopo la Mawakili wa Utetezi aliomba kuwasilisha ombi.

Aliiomba Mahakama ifute shitaka la utakatishaji wa fedha kwa kuwa lina mapungufu makubwa ya kisheria ambayo hayawezi kurekebishwa wala kufumbiwa macho isipokuwa kufutwa.

Alidai ili shitaka liwe la utakatishaji wa fedha lazima kuwa na dhamira ya kuficha chanzo cha fedha au lengo la washitakiwa kukwepa adhabu lakini kama hakuna mambo hayo sheria inatoa mamlaka kwa Mahakama kuyafuta mashitaka hayo.

Upande wa Jamhuri uliiomba Mahakama iahirishe kesi hiyo ili wajiandae kujibu hoja za upande wa utetezi. Hakimu Mashauri alikubali ombi hilo na kuahirisha kesi hiyo hadi kesho kwa ajili ya kusikiliza majibu ya Jamhuri.


Washitakiwa wote walirudishwa rumande kwa kuwa mashitaka yanayowakabili hayana dhamana. Mbali na mashitaka hayo, Choma anakabiliwa na kesi nyingine yenye mashitaka 199 ya kuisababishia serikali hasara ya Sh bilioni 15.6 katika mahakama hiyo.
Viewing all 7853 articles
Browse latest View live