Rais Magufuli mchana huu analizindua rasmi Bunge la 11 la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania mjini Dodoma ambapo pia atatoa mwelekeo wa Serikali yake ya Awamu ya Tano katika miaka mitano ijayo.
Kabla ya kuingia ndani ya ukumbi wa Bunge, Rais amekagua gwaride maalumu lililoandaliwa kwa ajili
Awali, kabla ya Rais Magufuli kuingia Bungeni,Mwanasheria Mkuu wa Serikali, George Masaju alitoa hoja ya kutengua kanuni ili kuwaruhusu viongozi wa kitaifa kuingia bungeni kushuhudia Rais Magufuli akihutubia Bunge.
Tundu Lissu: Napenda tupate muongozo kuhusu baadhi ya wageni kuwakaribisha ndani, kwa hali ilivyo leo hatuna Rais wa Zanzibar, hatuna makamu wa kwanza au wa pili halali wa Zanzibar, hatuna spika wala baraza la wawakilishi Zanzibar.
Kwa mujibu wa katiba ya Zanzibar muda wa serikali ya Zanzibar uliisha tangu Novemba 2.
Naibu spika amemjibu kwa kusema kifungu pia kinasema Rais wa Zanzibar anafikia ukomo mpaka Rais mpya anapoapishwa.
Update
Muda huu Rais wa Zanzibar ndo anaingia Bungeni,lakini kuna hali ya vurugu. Wabunge wa Ukawa wanazomea huku wakisema Maalim Seif...... Maalim Seif........Maalim Seif.......Maalim Seif
--> Wabunge wa CCM nao wanashangilia huku wakisema CCM......CCM....CCM
Kwa mujibu wa katiba ya Zanzibar muda wa serikali ya Zanzibar uliisha tangu Novemba 2.
Naibu spika amemjibu kwa kusema kifungu pia kinasema Rais wa Zanzibar anafikia ukomo mpaka Rais mpya anapoapishwa.
Update
Muda huu Rais wa Zanzibar ndo anaingia Bungeni,lakini kuna hali ya vurugu. Wabunge wa Ukawa wanazomea huku wakisema Maalim Seif...... Maalim Seif........Maalim Seif.......Maalim Seif
--> Wabunge wa CCM nao wanashangilia huku wakisema CCM......CCM....CCM