Quantcast
Channel: LEWIS MBONDE BLOG
Viewing all articles
Browse latest Browse all 7853

Rais Magufuli Yuko Bungeni Muda Huu Kwa Ajili Ya Kulizindua na Kuhutubia

$
0
0

Rais Magufuli mchana huu   analizindua  rasmi  Bunge  la  11  la  Jamhuri  ya  Muungano  wa  Tanzania  mjini Dodoma ambapo pia atatoa mwelekeo wa Serikali yake ya Awamu ya Tano katika miaka mitano ijayo.

Kabla  ya  kuingia  ndani  ya  ukumbi  wa  Bunge,  Rais  amekagua  gwaride  maalumu  lililoandaliwa  kwa  ajili
 

Awali, kabla  ya  Rais  Magufuli  kuingia  Bungeni,Mwanasheria Mkuu wa Serikali, George Masaju alitoa hoja ya kutengua kanuni ili kuwaruhusu viongozi wa kitaifa kuingia bungeni kushuhudia Rais Magufuli akihutubia Bunge.

Tundu Lissu: Napenda tupate muongozo kuhusu baadhi ya wageni kuwakaribisha ndani, kwa hali ilivyo leo hatuna Rais wa Zanzibar, hatuna makamu wa kwanza au wa pili halali wa Zanzibar, hatuna spika wala baraza la wawakilishi Zanzibar.

Kwa mujibu wa katiba ya Zanzibar muda wa serikali ya Zanzibar uliisha tangu Novemba 2.

Naibu spika amemjibu kwa kusema kifungu pia kinasema Rais wa Zanzibar anafikia ukomo mpaka Rais mpya anapoapishwa.


Update
Muda  huu  Rais  wa  Zanzibar  ndo  anaingia  Bungeni,lakini  kuna  hali  ya  vurugu. Wabunge  wa  Ukawa  wanazomea  huku  wakisema  Maalim Seif...... Maalim Seif........Maalim Seif.......Maalim Seif

--> Wabunge  wa  CCM  nao  wanashangilia  huku  wakisema  CCM......CCM....CCM 

Viewing all articles
Browse latest Browse all 7853

Trending Articles