
Leicester City wameshinda ndoo ya Premier League na kuweka bonge la historia kwenye kwenye mchezo wa soka ya muda wote.
Sare ya bao 2-2 kati ya Chelsea vs Tottenham Jumatatu usiku, ilipeleka mafaniko makubwa kwenye kikosi cha Claudio Ranieri.
Leicester ilianza msimu huu ikiwa na presha ya kunusurika kushuka daraja msimu uliopita na haikuwa ikiwaziwa kama ingeweza kuchukua ndoo katika historia ya soka la England.
Wapinzani wake wa karibu katika harakati za kuwania taji hilo Spurs, Arsenal, Manchester City, Manchester United pamoja na mabingwa watetezi Chelsea wote wamechemka kuwa na mwendelezo mzuri wa matokeo kama Leicester kwenye msimu huu.