
Jumamosi ya September 26 ni siku ambayo ilikuwa ikisubiriwa kwa hamu na mashabiki na wapenzi wa soka Tanzania, kwani ndio siku ambayo tumepata nafasi ya kuona mechi ya kihistoria ya watani wa jadi Simba dhidi ya Yanga mchezo uliochezwa uwanja wa Taifa Dar Es Salaam.
Kabla ya kuchezwa kwa mechi hiyo ya kihistoria ambapo klabu ya Simba ndio ilikuwa timu mwenyeji wa mchezo huo, Simba na Yanga wamewahi kukutana mara 79, lakini klabu ya Dar Es Salaam Young Africans kwa mujibu wa rekodi inaonekana kuwa mbabe kwa kuifunga Simba mara 29, huku Simba wakiwa wamewahi kuifunga Yanga mara 23 na kutoka sare mara 27. Hii ndio rekodi ambayo Simba na Yanga ziliingia uwanjani zikiwa zinaijua.
Mchezo umemalizika kwa klabu ya Dar Es Salaam Young Africans